Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Afya Bukene kitapatiwa mashine ya x- ray na ultrasound?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMAN J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Tangu mashine hii ya Ultrasound ifungwe pale Bukene, hakujawahi kuwa na mtaalam wa hii mashine, na kwa hiyo, wagonjwa wanapofika pale hawapati huduma hii, na badala yake wanapelekwa Kituo cha Afya cha Itobo kilichopo zaidi ya kilometa 20: Je, Serikali inaweza kutoa maelekezo maalum kwa Mganga Mkuu wa Halmashauri au Wizarani ili mtaalam wa Ultrasound apelekwe, awe station pale kwa sababu hakuna tija yoyote kuwa na mashine ya Ultrasound wakati mtaalam wa kuiendesha hayupo na, kwa hiyo haifanyi kazi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa jengo mahususi kwa ajili ya kuweka mashine ya X-Ray katika Kituo cha Afya cha Itobo linakamilika; je, ni nini commitment ya Serikali sasa ya kuweka mashine hiyo mara tu jengo hilo litakapokamilika pale Kituo cha Afya cha Itobo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Suleman Jumanne Zedi, Mbunge wa Jimbo la Bukene, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali imepeleka mashine ya Ultrasound katika Kituo cha Afya hiki cha Bukene, lakini safari ni hatua. Tulianza kwanza kuandaa mazingira kwa maana ya kandaa majengo na kupeleka mashine. Sasa hatua inayofuata ni kupeleka mtaalam wa mashine ya Ultrasound ili aanze kutoa huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshatoa maelekezo. Nitumie fursa hii kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nzenga kuangalia ndani ya wilaya kufanya internal redistribution ya staff kwa ajili ya kwenda kutoa huduma ya Ultrasound, na Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutaangalia uwezekano wa kupata mtaalam mwingine kwa ajili ya kwenda kuongeza nguvu kule Bukene.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuhusiana na Jengo la X-Ray katika Kituo cha Afya cha Itobo, ni kweli Serikali inaendelea na ujenzi na mara baada ya kukamilika jengo lile, mashine ya X- Ray itapelekwa ili tuendelee kutoa huduma kwa wananchi wa Itobo, ahsante.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Afya Bukene kitapatiwa mashine ya x- ray na ultrasound?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kituo cha Afya Mlalo ni miongoni mwa vituo vikongwe kabisa ambavyo havina huduma ya X-Ray: Je, ni lini Serikali itahakikisha sasa kituo hiki kinapata huduma hiyo ya X-Ray kwa sababu kinahudumia zaidi ya kata tisa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rashid Shangazi, Mbunge wa Jimbo la Mlalo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vyetu vyote vya afya kote nchini vimewekwa kwenye mpango mkakati wa kujenga majengo kwa ajili ya huduma za upimaji na huduma za X-Ray na Ultrasound zikiwemo. Kwa hiyo, naomba nilichukue hili ili tuweze kufanya tathmini kwenye Kituo hiki cha Afya cha Mlalo tuone uwezekano wa kupata fedha kwa ajili ya kujenga Jengo la X-Ray na baadaye kuweka mashine kwa ajili ya kuendelea kutoa huduma, ahsante.