Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga majengo ya kisasa katika Vituo vya Afya vya Kinyangira na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Serikali yanayojaribu kuwafariji wananchi wa Kinyangiri na Mkalama nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Kinyangiri ni cha enzi ya ukoloni, ni kituo cha siku nyingi sana na kinahudumia Tarafa nzima, kilipelekea mpaka kiongozi mkubwa wa chama kinachounda Ilani kuwaahidi wananchi wa Kinyangiri kwamba ifikapo Disemba kama hawajapata majengo waandamane ofisini kwake. Serikali na Wizara ina kauli gani kuhusu kauli hii nzito ya Kiongozi mkubwa wa chama kinachounda Ilani?

Swali la pili; Kituo cha Afya Mkalama pia ni cha wakati wa ukoloni hakina uwezo hata wa kufunga P.O.P kama mtu amevunjika mkono au mguu, hivyo wananchi wanateseka na kinahudumia wananchi takribani 15,000. Serikali ina- commitment gani kuhusiana na bajeti hii inayokuja kuhusiana na Kituo hiki cha Afya cha Mkalama? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Kituo cha Afya cha Kinyangiri ni kituo chakavu na kituo kongwe, Serikali imeshaweka mpango wa kutafuta fedha ili kwenda kukikarabati pia kuongeza majengo ambayo yanapungua. Nimhakikishie kwamba Serikali hii kwa sababu inatekeleza Ilani cha Chama cha Mapinduzi na Kiongozi wetu alifika pale na kutoa maelekezo hayo, tunachukua maelekezo hayo na tunaanza kuyafanyia kazi kuhakikisha tunapata fedha kwa ajili ya kituo cha Kinyangiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Pili; kuhusiana na kituo cha afya cha Mkalama ambacho nacho ni chakavu tutaendelea kutenga fedha kwa awamu ili tuweze kuvikarabati vituo kama hivi pia kuongeza miundombinu ambayo inakosekana. Ahsante.