Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 55 2023-04-12

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga majengo ya kisasa katika Vituo vya Afya vya Kinyangira na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI) naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kujenga na kukarabati vituo vya afya kwenye Kata za kimkakati ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetoa fedha shilingi bilioni 117 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya 234 kwenye Tarafa na Kata za kimkakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vituo vya Afya vya Kinyangiri na Mkalama ni miongoni mwa vituo vinavyoendelea kutoa huduma katika ngazi ya Kituo cha Afya pamoja na changamoto ya upungufu wa miundombinu hususan ya upasuaji wa dharura.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya nchini kote vikiwemo vituo vya afya Kinyangiri na Mkalama. Ahsante.