Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaajiri walimu wanaojitolea katika Jimbo la Kiteto?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa majibu ya Serikali.

Swali la kwanza; kwa kuwa Kiteto ina upungufu wa walimu karibu 800 ukichanganya shule za msingi na sekondari. Kwa hivyo kama isingekuwa siyo hawa 120 hali ingelikuwa mbaya; je, ni lini ni lini Serikali italeta Sheria ya Ajira hapa tuweke kigezo cha kujitolea iwe ni sababu ya mtu kuajiriwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; ni lini Mheshimiwa Waziri atakuja Kiteto akutane na Walimu hawa wazalendo wanaojitolea wanaojitolea ili azungumze nao? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Edward Kisau Olelekaita, Mbunge wa Jimbo la Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Halmashauri ya Kiteto ina upungufu wa walimu, lakini niwapongeze Halmashauri ya Kiteto kwa kuweka bajeti angalau kidogo kwa ajili Walimu wanaojitolea. Nimhakikishie kwamba Serikali imeweka mpango na mwongozo kwa ajili ya kuwawezesha Walimu wanaojitolea kutambulika rasmi, lakini pia kupewa kipaumbele wakati fursa za ajira zinapojitokeza na kwa kuwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo kupitia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ametangaza jumla ya ajira 21,200 za Kada ya Elimu lakini pia na Kada ya Afya, niwatie shime hawa Walimu wanaojitolea Kiteto na maeneo mengine kuomba ajira hizo ili waweze kupewa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili kuhusiana na kukutana na Walimu hawa sisi tuko tayari baada ya shughuli hizi za Bunge, basi tuambatane na Mheshimiwa Mbunge, ili tuweze kuonana na Walimu hao na kuwatia moyo kufanya kazi nzuri, ahsante.