Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 53 2023-04-12

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawaajiri walimu wanaojitolea katika Jimbo la Kiteto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshiwa Edward Kisau Olelekaita, Mbunge wa Jimbo la Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ina jumla ya walimu 752 wa shule za msingi na walimu wa kujitolea 86. Aidha, kwa shule za sekondari kuna jumla ya walimu 298 na walimu wa kujitolea 34.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa Walimu wa kujitolea katika shule za msingi na sekondari na kwa kuwa Serikali huajiri kulingana na upatikanaji wa fedha. Hivyo nafasi za ajira zikitangazwa, tunawashauri Walimu hawa wanaojitolea waombe nafasi hizo ili wale wanaokidhi vigezo waweze kuajiriwa kwa kupewa kipaumbele, ahsante.