Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Wanawake wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo wa madini?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri, kuhusiana na wanawake wanaoshiriki katika madini Mkoa wa Arusha lakini naomba kuuliza maswali mawili.

Swali la kwanza; wanawake wanapojishughulisha na shughuli za madini Mkoani Arusha wanakutana na changamoto nyingi sana; je, ni nini Mkakati wa Serikali wa kutatua changamoto zinazowakabili wanawake?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Wilaya ya Ngorongoro yamegundulika madini mengi, lakini inaonekana kwamba wanawake hakuna mazingira yanayowawezesha kushiriki katika shughuli za madini. Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba maeneo ya madini kwenye Wilaya ya Ngorongoro yanapimwa ili wanawake nao waweze kushiriki ipasavyo katika shughuli hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Ole–Shangai, Mbunge wa Ngorongoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa changamoto za wanawake Serikali imeendelea kutoa elimu, kuwahamasisha wajiunge na vikundi mbalimbali ambavyo nimevitaja kwenye swali la msingi ili waweze kusaidiwa kupata elimu juu ya sheria, kanuni na taratibu za madini pamoja na kufahamu fursa za biashara na uwekezaji kwenye sekta ikiwa ni pamoja na kuelekeza namna ya kupata mitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili kuhusu Wilaya yake ya Ngorongoro, ni kweli kwanza nimpongeze Mbunge maana yake mwisho wa mwezi uliyopita aliniomba nifanye Wizara kwenye Jimbolake ili kwenda kubaini changamoto zinazowakabili wachimbaji wa madini. Tukagundua kwamba Ngorongoro ina madini mengi sana ya vito, lakini uendelezaji wa sekta uko chini sana hasa kwa upande wa wanawake. Nitumie fursa hii kumhakikishia kwamba baada ya ziara ile tuliagiza Taasisi yetu ya Jiolojia na Utafiti wa Madini pamoja na Tume ya Madini waende kule wakahamasishe ile jamii na wabainishe maeneo yenye madini ili wanawake nao wa Ngorongoro wajiunge waweze kufaidi fursa hii iliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatukuishia hapo, Wizara hii imeteua Mabalozi wa Madini, wanawake wanaongozwa na Dkt. Ritta Kabati ambao kazi yao ni kuwahamasisha wanawake wote wanaopenda kujiingiza katika biashara ya madini, wafahamu biashara ya madini na fursa zilizoko za wawekezaji, ahsante sana. (Makofi)

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Wanawake wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo wa madini?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nataka kufahamu ni lini Serikali itaipatia Kampuni ya Peak Resources leseni? Ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba utaratibu wa kupata leseni za madini uko katika mfumo wa kieletroniki na mfumo huo unafikika kwa njia ya kimtandao. Baada ya mtu kuingia kwenye mtandao na akaomba leseni utaratibu mzima wa jinsi ya kujaza fomu, ada zinazohitajika unalipiwa kimtandao na kwa kawaida kama mifumo iko sawa na hakuna break down kwenye system ndani ya wiki, mbili leseni huwa zinatoka, lakini kama kuna changamoto kwenye leseni yoyote, Ofisi yetu ya Madini iko wazi saa zote na tuko tayari kutoa ushirikiano ili leseni anayoisemea iweze kupata.