Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Madini 66 2023-04-12

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL L. SHANGAI K.n.y. MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Wanawake wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo wa madini?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Wazari wa Madini, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake wamekuwa wakishiriki kwa kiasi kikubwa kwenye sekta ya madini kupitia vyama mbalimbali ikiwemo Shirikisho la wachimbaji wadogo nchini (FEMATA) lenye lengo la kuwaunganisha wachimbaji wadogo wa madini wakiwemo wanawake pia Umoja wa Wanawake Wachimbaji Madini (TAWOMA) ambao unajumuisha wanawake wote wanaojishughulisha na shughuli za uchimbaji na utengenezaji bidhaa mbalimbali zinazotokana na madini. Pia wako Muungano wa Wanawake Wanaouza Bidhaa Mbalimbali Migodini (WIMO) na Chama cha Tanzania Women in Mining and Mineral Industry (TWIMMI) ambacho kimeundwa kwa lengo la kuwaweka pamoja wachimbaji wa madini wanawake na wote walioko kwenye sekta ya madini ili kuweka mazingira bora ya kuwawezesha wanawake na ustawi wa sekta ya madini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali na uwepo wa vyama hivyo Wizara imekuwa ikisaidia wanawake kwenye sekta ya madini katika mnyororo mzima kwa kuwapa leseni za uchimbaji, uongezaji thamani na uuzaji madini, ahsante sana.