Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itabadili majina ya kigeni kuwa ya Kitanzania kwenye rasilimali za Taifa ikiwemo Mlima Livingstone na Ziwa Victoria?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Mheshimiwa Waziri amezungumzia suala la historia, simba wa jina la Bob Junior aliyekufa siku za karibuni tumeona mataifa mbalimbali, vyombo vya habari zikichukua habari zake kama simba ambaye ni shujaa. Hivi ni kweli hatuna mashujaa hapa Tanzania ambao watapewa majina kama huyo simba aliyekufa? Ambaye pia watoto wake wanaitwa Rihana na majina mengine ya kizungu, hatuna watu mashuhuri kama kina Mkwawa, akina Mwansasu, aakina Mwakatumbula wakapewa majina hayo na mwisho tukaweza kufanikiwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; ukishasoma historia Livingstone na majina mengine kama hayo tuna Machifu katika maeneo yale ambao wangeweza kupewa majina yao. Je, ni lini Serikali italeta Muswada wa kubadilisha majina kama hayo yaliyopewa wakati wa kikoloni ili watu wetu waweze kupewa hizo nafasi na majina yao ya Kiafrika yakasimama zaidi? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimkumbushe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba utalii wa Tanzania au utalii wowote hapa duniani ni utalii unaohusisha wazawa kwa maana ya wenyeji, lakini pia na watalii wa nje. Tunapotumia majina maarufu hatutangazii Watanzania peke yake, tunatangazia ulimwengu, kwa hiyo hiyo historia inabebwa kiulimwengu. Kwa mfano tuna mchukulia Bob Junior ambaye ni simba ambaye amekufa hivi karibuni na alikuwa na watoto wake mmoja alikuwa anaitwa Rihana. Tunapotumia jina Rihana ina maana hata mtalii anetoka Marekani anaweza kuja kumwangalia Rihana, lakini tutakapompa let say Masanja, aliyesimama hapa watakao mfahamu wa hapa hapa Tanzania, kwa hiyo tunatangaza utalii duniani ili kuonyesha jinsi gani Watanzania tumejaliwa na rasilimali tulizonazo hapa nchini, ahsante. (Makofi)