Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 67 2023-04-12

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itabadili majina ya kigeni kuwa ya Kitanzania kwenye rasilimali za Taifa ikiwemo Mlima Livingstone na Ziwa Victoria?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo baadhi ya Rasilimali za Taifa zenye majina na maeneo ambayo zilipewa tangu kipindi cha utawala wa ukoloni. Majina hayo yalitolewa kutokana na juhudi za waasisi katika ulinzi na uhifadhi wa rasilimali hizo. Majina na maeneo hayo yameendelea kufahamika kihistoria kutokana na kutangazwa na Taifa na kuandikwa kwenye nyaraka na vitabu mbalimbali na rasilimali hizo zimeendelea kuhifadhi historia ya nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na umuhimu wa rasilimali hizo kwa historia ya nchi yetu na kuendelea kufahamika zaidi kitaifa na kimaitafa pasipokuwa na changamoto yoyote, Serikali haioni haja ya kubadili majina na maeneo hayo ambayo kwa sasa yana mchango mkubwa kiuchumi kwa Taifa letu. Aidha, Serikali kwa sasa inaendelea pia kuzingatia majina ya wazawa kwenye rasilimali mbalimbali za Taifa kadiri zinavyoanzishwa.