Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Mradi wa Maji Kabanga?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana; pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri mimi nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, mkandarasi wa mradi huo wa Kabanga hajalipwa fedha zake kwa mwaka mzima. Naomba kujua ni sababu gani zimesababisha mkandarasi huyu asilipwe fedha yake kwa mwaka mzima?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; naomba kujua, Wizara ya Maji na Serikali wana mfumo wa kuweza ku-track status ya miradi ya maji ili kuepukana na changamoto hizi za miradi kusimama na mkandarasi kutokuwa site kwa mwaka mzima? Naomba kupata majibu ya Serikali ya maswali hayo mawili.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niendelee kuwaomba tu wakandarasi ambao wanaidai Serikali kwamba kwa sasa Serikali imeshaanza kulipa na tayari fedha zimeshaanza kupelekwa katika maeneo husika. Kwa hiyo wakae mkao wa kupokea fedha hizo ili waweze kuendelea na kazi ambazo ziko katika site hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye upande wa strategy, tunaamini kwamba lengo la Serikali ni kumtua ndoo mama kichwani, na strategy mojawapo ni kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi kwa ukaribu zaidi. Hivyo nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa Serikali imeshaweka mikakati mahususi ya kuhakikisha maji haya yanawafikia wananchi tutaendelea kusimamia kwa ukaribu zaidi ili miradi hii iweze kukamilika na wananchi waweze kupata huduma iliyo bora.