Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 64 2023-04-12

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Mradi wa Maji Kabanga?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Mradi wa Maji Kabanga unaendelea kwa gharama ya Shilingi 941,351,342.74. Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 75 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Juni, 2023 na kuhudumia wananchi zaidi ya 15,000 wa Vijiji vya Kabanga, Murukukumbo na Kumwuzuza. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa dakio, nyumba ya mashine, tanki la kukusanyia maji lenye ujazo wa lita 120,000, tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 230,000 na ujenzi wa viosk vitatu. Kazi zinazoendelea ni pamoja na uchimbaji wa mitaro kwa ajili ya kulaza mabomba umbali wa kilometa 20.694 na ukamilishaji wa ofisi ya CBWSO.