Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y. MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima wa Tarime wanaolima kahawa aina ya Arabika?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana; zao la kahawa limevamiwa na ugonjwa wa mnyauko ambao unaweza ukasababisha zao hili kutoweka zao hili muhimu: -

Je, Serikali imechukua hatua gani za haraka ili kulinda zao hili muhimu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; zao la kahawa ni zao la kimkakati lakini bado halijaweza kumnufaisha mkulima ipasavyo: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka masoko mazuri ambayo yatamnufaisha mkulima apate bei nzuri?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali la kwanza, kahawa inaathiriwa na magonjwa makubwa matatu chulebuni, kutu ya majani pamoja na mnyauko fuzari. Mnyauko fuzari ndio umekuwa ni changamoto kubwa sana. Hatua ambazo tumezichukua, kituo chetu cha utafiti wa zao la kahawa TaCRI hivi sasa kinakuja na variety mpya ambayo itakuwa ni himilivu katika magonjwa, hasa ugonjwa huu wa mnyauko fuzari. Pia tumeendelea kutoa elimu kwa wakulima juu ya kufanya palizi ; kwa sababu moja ya changamoto kubwa ni mashamba kuwa machafu, vilevile kung’oa miche yenye changamoto na isipandwe kabla ya miezi sita ndio elimu tumekuwa tukizitoa.