Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 63 2023-04-12

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y. MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wakulima wa Tarime wanaolima kahawa aina ya Arabika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Bodi ya Kahawa inaendelea kukiwezesha na kukiongezea uwezo Kituo Kidogo cha Utafiti wa Kahawa (TaCRI) kilichopo eneo la Nyamwaga Tarime ili kuzalisha miche milioni moja kwa mwaka. Miche hiyo inaendelea kuzalishwa na kusambazwa bure kwa wakulima wa Kahawa Wilaya ya Tarime na Wilaya nyingine za Mkoa wa Mara. Kupitia jitihada hizi kuanzia mwezi Septemba, 2022 hadi kufikia mwezi Machi, 2023 jumla ya miche 173,471 imezalishwa na kugawiwa bure kwa wakulima. Aidha, Serikali imeboresha mfumo wa masoko kwa kuwezesha kuanza kufanya kazi kwa mitambo ya kuchakata kahawa katika maeneo ya Muriba na Nyantira.