Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukiongezea mtaji kiwanda cha Kahawa cha TANICA?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana; Mkoa wa Kagera unafahamika kwa uzalishaji wa zao la kahawa, na ni zao la kimkakati, na Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imejikita kuboresha na kuongeza thamani ya zao la kahawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya wabia wa Kiwanda cha TANICA Serikali ni mbia na kuna hisa za zaidi bilioni 8.6 ambazo hazijalipiwa. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakisha kwamba hizo hisa ambazo hazijalipiwa za bilioni 8.6 zinalipiwa ?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, Serikali iliunda kamati maalum kwa ajili ya kuangalia namna ya kukikwamua kiwanda hiki muhimu sana cha kuzalisha kahawa katika Mkoa wa Kagera; hivyo tuko katika hatua za mwisho za kuona namna gani ya kupata fedha hizo pia kuona wanahisa wanaongeza hitaji ili, moja, kupata hizo fedha ambazo ni mtaji muhimu pili, kupata teknolojia ya kisasa ambayo itasaidia uzalishaji wenye tija wa kiwanda hicho; kwa sababu moja ya changamoto tuliyonayo ni uchakavu wa mitambo au mashine zilizofungwa tangia mwaka 1967.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Serikali inafanyia kazi na fedha zitakazopatikana tutaweza kuboresha kiwanda hiki pia kuhakikisha uzalishaji unakuwa na tija kwa ajili ya manufaa Taifa hili na Mkoa wa Kagera, nakushukuru.