Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 62 2023-04-12

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukiongezea mtaji kiwanda cha Kahawa cha TANICA?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua mwenendo wa kibiashara usioridhisha wa Kiwanda cha Tanganyika Instant Coffee Company Limited (TANICA) unaochangiwa na changamoto ya ukosefu wa mtaji, uchakavu wa mitambo, matumizi ya teknolojia iliyopitwa na wakati na kiwanda kuwa na madeni makubwa. Kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina, Serikali imefanya upembuzi yakinifu wa mahitaji ya rasilimali fedha kwa ajili ya kuendesha kiwanda hicho, ambapo imebainika kuwa zinahitajika takribani dola za Marekani milioni 1.31.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Serikali inafanya mashauriano na wanahisa wa kiwanda ili wawekeze kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kukiboresha na kuendesha kiwanda hicho. Serikali ina nia ya dhati kuhakikisha kuwa kiwanda hicho kinafanya kazi kwa ufanisi na tija ili kuendeleza zao la kahawa ambalo linalimwa kwa wingi katika Mkoa wa Kagera, nakushukuru.