Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza Watumishi wa Afya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kumshukuru sana Waziri kwa majibu yake mazuri. Nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Busega na Wilaya Itirima tuna hospitali nzuri sana za wilaya, tatizo ni moja majengo ni mazuri na yanapenda hatuna watumishi wa kutosha. Kwa hiyo hospitali zile hazina hadhi ya kuitwa hospitali ya wilaya kwa sababu watumishi hawatoshi;

Je ni lini Serikali itapeleka watumishi wa kutosha ili na wananchi wa kule wafaidike?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge jinsi anavyofuatilia masuala ya afya kwenye mkoa wake kwa kushirikiana na Wabunge wa majimbo. Kama ambavyo nimesema kwamba kwa mwaka huu tunategemea kupata watumishi takribani 12,000 hivi. Tutaendelea kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ili tuweze kuona ni namna gani tunaweza kupeleka watumishi maeneo hayo ili wananchi waweze kupata huduma kulingana na ukubwa wa hospitali yenyewe.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaongeza Watumishi wa Afya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu?

Supplementary Question 2

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina changamoto kubwa sana ya watumishi kada ya elimu na afya;

Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ili kuondoa changamoto iliyopo hasa ukizingatia Ukerewe ni kisiwa ambacho kimejitenga na wananchi wake wanapata shida sana?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuuliza swali zuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, si tu suala la watumishi kwenye Kisiwa cha Ukerewe, tumeamua kama Wizara ya Afya tuchukulie Ukerewe kama kanda maalum; na ndiyo maana Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe sasa inaenda kupewa hadhi kama hospitali ya mkoa. Maana yake ni kwamba sasa yenyewe haitaenda kupata watumishi na vilevile vifaa tiba na mambo mengine kama hospitali ya wilaya bali inaenda kupata kama hospitali ya mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunajua kwamba kuna visiwa mbalimbali; ukisema umemaliza kijiji kimoja kumbe kijiji hicho kina visiwa mbalimbali. Maana yake ni kwamba ukizungumzia zahanati hutaenda kufikiria Ukerewe ukasema kijiji ukadhani umemaliza. Tunatamani kila kisiwa kiwe na zahanati yake kwa ajili ya logistic zilizopo kule. Kwa hiyo tunachukua tutashirikiana na wewe Mbunge na Mbunge wa Jimbo tuhakikishe tumefikia azma yenu ambayo mnaitamani.