Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 61 2023-04-12

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaongeza Watumishi wa Afya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu mwaka 2018 ilikuwa na watumishi 130. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Wizara iliwapanga watumishi 70 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu na kuhamisha wengine 18 hivyo kufanya jumla ya watumishi kuwa 218.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuwapanga watumishi katika mikoa hii ya pembezoni mwa nchi ili kufikia malengo kwa kadri tutakapokuwa tunapata vibali vya kuajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.