Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo kipya cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni pamoja na kupeleka samani?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina swali dogo tu la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni awamu ya pili hii kuambiwa tumetengewa fedha kwa ajili ya ukarabati wa kituo hiki. Na kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba kwa kweli uchakavu ni wa hali mbaya sana. Tunaomba commitment ya Serikali; kama ni kweli kituo hiki kitajengwa kwenye bajeti ya mwaka unaokuja, ni quarter ipi wamepanga kufanya ukarabati wa kituo hiki?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kombo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, atakumbuka Mheshimiwa Kombo kwamba nilitembelea Kituo hiki cha Micheweni nikajionea hali halisi; na kwa msingi huo tukakubaliana ndani ya Wizara na Jeshi la Polisi kutenga fedha. Atakumbuka kwamba miaka iliyopita hata kama alipewa ahadi hakuna fedha iliyotengwa lakini mwaka ujao namhakikishia fedha imetengwa na tutahakikisha tutakapopata fedha za maendeleo basi kituo hiki tutakipa kipaumbele, nashukuru.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo kipya cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni pamoja na kupeleka samani?

Supplementary Question 2

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kituo cha Polisi Mji Mdogo wa Mpui na Kaengesa vimechakaa sana na vinahudumia kata 11.

Je, ni lini Serikali inakarabati vituo vya polisi katika mji mdogo wa Kaengesa na Mpui?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deus kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake ameliuliza kwa ujumla, kwamba ni lini Serikali itakarabati vituo vilivyochakaa kama ilivyo cha kwakwe cha mji mdogo alioutaja. Nimuahidi tu kwamba pale tutakapokuwa tunapata fedha na vituo hivi vikiingizwa kwenye bajeti basi vitafanyiwa ukarabati. Atakumbuka kwamba mwaka huu maeneo mengi ikiwemo hata Zanzibar na Bara baadhi ya vituo vimekarabatiwa. Kwa hivyo nimwahidi tu kwamba kadri hali ya fedha itakavyoruhusu kituo chake pia kitafanyiwa ukarabati, nashukuru.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo kipya cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni pamoja na kupeleka samani?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Wananchi wa Kata ya Nanjirinji wakishirikiana na mimi Mbunge wao wamejenga na kukamilisha kituo cha polisi ili kupunguza uhalifu mkubwa katika eneo la Nanjirinji. Je, Serikali iko tayari sasa kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani kuelekeza uongozi wa polisi Mkoa wa Lindi wakakague kituo hiki wafanye tathmini na hatimaye kupanga askari wakafanye kazi pale?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Kassinge kwa kujumuika na wananchi wake wakajenga na wakakamilisha kituo cha polisi kama ilivyoelezwa hapa Bungeni. Ni maelekezo yangu kwa IGP kupitia Kamanda wake wa Polisi wa Mkoa wafanye ukaguzi wa kituo hiki ili kama kina kidhi haja kiweze kupangiwa askari na kuanza kuwahudumia wananchi wa eneo hilo, nashukuru.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo kipya cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni pamoja na kupeleka samani?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana; Wilaya ya Skonge tangu ianzishwe mwaka 1996 OCD amejibanza kwenye vijumba ambavyo vilianzishwa na Mtemi Haruna Msagila Lugusha, 1957, havitoshi na havifai;

Je, Wilaya ya Skonge itajengewa lini kituo cha polisi cha Wilaya chenye hadhi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Kakunda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tuungane naye kwamba baadhi ya majengo yanayotumika na polisi si yale yaliyojengwa na Serikali bali ni yale yaliyotolewa na wadau waliokuwa kwenye maeneo hayo miaka kadhaa iliyopita. Sasa kupitia Bunge lako Tukufu nimwombe IGP kupitia RPC wake wa Mkoa wa Tabora waweze kufanya tathmini ya eneo hilo la kibanda anachosema kinakaliwa na OCD wa Sikonge kuangalia kiwango gani cha ukarabati tunahitajika kufanyika ili tukitengee fedha kikarabatiwe kikidhi mahitaji ya OCD, nashukuru.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo kipya cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni pamoja na kupeleka samani?

Supplementary Question 5

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, kwamba maeneo mengi yaliyojengwa vituo vya polisi ikiwemo kituo kikuu cha polisi pale Nyegezi ambacho kitasaidia maeneo mengi sana, kwa maana ya ukanda wa kata za Buhongwa, Mkolani, Ruanima, Nyegezi, Luchelele pamoja na Mkolani yenyewe.

Je, ni lini sasa Serikali itafanya ukamilishaji wa kituo hiki?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mabula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nielekeze Mkuu wa Polisi Nchini (IGP) Wambura kupitia Kamanda wake wa Mkoa wa Mwanza wapiti kituo hiki cha Nyegezi alichokieleza Mheshimiwa Mbunge kuona kiasi gani cha umaliziaji unaotakiwa kufanyika ili gharama zake ziweze kutengewa fedha na kikamilishwe ili kiweze kuwanufaisha wananchi wa maeneo yaliyotajwa.