Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 60 2023-04-12

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo kipya cha Polisi cha Wilaya ya Micheweni pamoja na kupeleka samani?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la mheshimiwa Omar Issa Kombo Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Micheweni ina kituo cha Polisi daraja B ambacho kinakidhi mahitaji ya kutoa huduma ya Polisi eneo hilo. Tatizo pekee la kituo hiki ni uchakavu unaohitaji kufanyiwa ukarabati. Tathmini ya uchakavu wa kituo imefanyika mwezi Januari 2023, na kubaini kuwa jumla ya shilingi 65,000,000 zinahitajika kwa ajili ya kubadilisha paa, dari, milango na madirisha, mfumo wa maji safi, maji taka, umeme, kuziba nyufa na kupaka rangi. Fedha hizo zimetengwa katika bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/2024 na kiasi cha fedha shilingi 17, 870,000 kwa ajili ya ununuzi wa samani za ofisi zinatarajiwa kuombwa kutoka kwenye mfuko wa tuzo na tozo kwa mwaka 2023/2024 mara ukarabati wa kituo utakapo kamilika.