Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza naishukuru Serikali kwa kuanza kumpata mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo lakini kwa kuwa kuna baadhi ya maeneo ambayo barabara hiyo imewafuata wananchi. Je, Serikali inampango gani kuhakikisha kwamba wananchi hao wanapewa fidia stahiki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa barabara hiyo ina urefu wa kilometa 79 na bado haijakamilika upembuzi yakinifu, Serikali inamkakati gani wa kuhakikisha kwamba inakamilisha upembuzi yakinifu kwa kilometa zote zilizobaki?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wananchi wa Jimbo la Vwawa kwamba tayari jedwali baada ya kuhakikiwa la malipo ya fidia kwa wale ambao barabara imefuata liko hazina kwa ajili ya uhakiki na hatua inayofuata sasa ni kwenda kufanya disclosure, yaani kuwaonyesha kila mtu atalipwa nini kwa maeneo ambayo bado. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi kwamba suala hili linaendelea na watalipwa hiyo fidia yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kukamilisha upembuzi na usanifu tuko kwenye hatua za mwisho kabisa kukamilisha usanifu ambapo ni hiyo Barabara ya Idiwili lakini Mahenge – Hasamba hadi Ileje.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kuuliza swali Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, ni kweli kwamba miradi ya barabara ile nane aliyoisema kwenye majibu yake ya msingi ikiwemo ya Masasi – Nachingwea itakayojengwa kwa program ya EPC + F ni kwamba haijulikani lini itaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hokororo, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakwenda na barabara hizi zote kwa pamoja na kama Mheshimiwa Mbunge alinisikiliza, hizi ni hatua na ni mfumo mpya. Kwa hiyo, kusema ni lini tarehe itakuwa ngumu lakini tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara ya Fedha sasa hivi inapitia kila barabara na kuona kwamba tunafanya tunavyotakiwa ili tutakapoanza kuzijenga hizo barabara tuwe na uhakika kwamba tulichofanya ni maamuzi sahihi na yatakwenda. Kwa hiyo, cha msingi tu ni kwamba ni hatua, ni process ambayo inaendelea lakini tutakapokuwa tumekamilisha upande huu tukishaanza kuitangaza sasa unaweza ukasema sasa baada ya kuitangaza tuna muda huu na huu.

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Barabara ya kutoka pale Nyashimo kwenda Dutwa yenye kilometa 47 tumekuwa tukiahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami zaidi ya miaka 10 sasa na kila nikiuliza toka nimekuja hapa Bungeni nimekuwa nikiambiwa kwamba itaanza kujengwa mwaka wa fedha ujao. Sasa naomba kuuliza ni mwaka wa fedha upi barabara hii sasa itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lusengekile, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema lakini kujenga kwa barabara pia kunategemea kwa kweli na upatikanaji wa fedha na mpango wa Serikali kwa kweli ni kuzijenga hizi barabara kwa kiwango cha lami ikiwepo na barabara ya Mheshimiwa Mbunge. Kwa hiyo, tunakwenda kwenye bajeti naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, kadiri muda unavyokwenda na kadiri tutakapoendelea kupata fedha barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nataka kujua ni lini Serikali itajenga kipande cha Barabara kutoka Mbande Kisewe mpaka Msongola ili kuunganisha Wilaya ya Temeke na Wilaya ya Ilala?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo, Mbunge wa Mbagala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama tulivyoongea barabara hii imeshakabidhiwa kwa Manager wa Mkoa wa Dar es Salaam kukamilisha hicho kipande kidogo sana ambacho kimebaki kwa kiwango cha lami.

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Mbinga – Litembo – Nkili ni barabara muhimu sana kwa wakulima wa kahawa. Nataka nipate majibu ya Serikali ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunda, Mbunge wa Mbinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyotaja itaanza kujengwa mara tu tutakapokuwa tumefanya review ama kukamilisha usanifu wa kina ikiwa sasa tutakuwa tumepata gharama ya hiyo barabara kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Kwa kuwa ipo Barabara ya Makondeko – Kwembe – Kisopwa hadi Mloganzila ya kilometa 14.66 imekuwa kwenye mpango na bajeti kwa miaka mitatu mfululizo. Je, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga kipande cha Makondeko kuelekea Kwembe hadi Kisopwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtemvu, Mbunge wa Kibamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Makondeko – Kwembe kwenda Kisopwa ni kati ya barabara ambazo zimejumuishwa kama barabara za kupunguza misongamano katika majiji. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge mpango upo wa kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Jimbo la Geita Vijijini wananchi wake hawajawahi kuona lami na tulipata lami kilometa 20 kutoka Nkome mpaka Kijiji cha Igate na upembuzi yakinifu tayari Mkandarasi tayari.

Je, ni lini mkandarasi huyo anaingia site kuanza kazi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Musukuma, Mbunge wa Geita kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tupo kwenye hatua za mwisho kabisa ili mkandarasi aweze kukabidhiwa hiyo site na nadhani Mheshimiwa Musukuma pia anajua kwamba taratibu zote karibu zimeshakamilika kwa hiyo kilichobaki tu ni hatua za mwisho ili mkandarasi aweze kukabidhiwa hiyo site.

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuniona.

Ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami kwa barabara inayotoka Singida Mjini – Ilongero – Mtinko mpaka Haydom kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ighondo, Mbunge wa Singida kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Singida – Ilongero inayoelekea Hydom tupo tunakamilisha usanifu wa mwisho. Tulifanya usanifu wa awali lakini sasa hivi tupo tunakamilisha usanifu na baada ya kupata hiyo detail design ndiyo sasa mipango ya kuijenga kwa kiwango cha lami itaanza.

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikushukuru, nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna barabara ambayo inatoka Mtwara Mnivata inayojengwa kwa kiwango cha lami kuelekea Newala mpaka Masasi. Kwa taratibu ambazo zinaendelea sasa hivi kuanzia Mnivata – Newala – Masasi wapo kwenye hatua za kulipa malipo kwenye zile nyumba ambazo zimeondolewa na miche. Lakini kipande cha kilometa 50 ambacho tayari kimejengwa barabara ya lami mpaka leo wananchi hawajalipwa fedha zao kama fidia. Je, ni lini Serikali itarudi kuwalipa fidia wananchi wale?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtenga, Mbunge wa Mtwara Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi barabara Mtwara – Mnivata imetekelezwa kwa fedha ya Serikali ya Tanzania na Barabara ya kuanzia Mnivata – Newala kwenda Masasi itatekelezwa kwa kusaidiana na wahisani ambao ni African Development Bank.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimwombe Mheshimiwa Mbunge kwamba kama kuna wananchi ambao katika eneo la Mtwara Mnivata bado wana changamoto ikiwa ni nje ya zile kilometa 45 tuweze kuonana nae ili niweze kupata taarifa kamili kwa wananchi ambao bado wanadai fidia eneo hili la Mtwara – Mnivata kilometa 50.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Barabara inayoanzia USA River kupitia Arusha National Park kwenda mpaka Oldonyo Sambu imejengwa kwa kiwango cha lami hadi kwenye lango la kuingia hifadhini.

Je, Serikali inampango gani wa kumalizia kipande kilichobaki kuanzia Ngarenanyuki kwenda Oldonyo Sambu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Arumeru kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, azma ya Serikali ni kukamilisha hicho kipande ambacho kimebaki lakini ukamilishaji wake pia utategemea na upatikanaji wa fedha na kwa kuwa tuko kwenye kipindi cha bajeti naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira tuone kama tutakuwa tumependekeza nini katika bajeti ambayo tunaiendea kuileta mbele ya Bunge lako.