Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 5 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 58 2023-04-12

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya kutoka njia panda ya Iyula – Idiwili - Nyimbili hadi Ileje itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Japhet Ngailonga Hasunga, Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imeanza kujenga barabara ya Njiapanda ya Iyula – Idiwili – Nyimbili hadi Ileje (kilometa 79) kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Mkandarasi amepatikana kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kilometa 2.1 kwa sehemu ya barabara ya kuanzia Njiapanda ya Iyula kuelekea Idiwili. Aidha, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu iliyobaki.