Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kukamilisha Ujenzi wa Mradi wa maji Tukuyu Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, kuna mradi wa Kiwira ambao naweza kusema ni mradi mama kwa sababu utawatua ndoo kichwani wanawake wengi wa Mkoa wa Mbeya. Mkandarasi alishasaini mkataba, lakini mpaka sasa hivi hajaanza kazi ya ujenzi wa mradi huo. Sasa je, ni lini mkandarasi huyo ataanza kazi rasmi ya ujenzi huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Tunaishukuru sana Serikali kwamba ilitoa ahadi ya kuleta fedha zaidi ya Shilingi bilioni nane kwenye mradi wa Kyela Kasumulu, mradi huo ambao utawasaidia wananchi wa Kata ya Nkuyu, Ndandalo, Mbugani, Kajunjumele, Bondeni, Serengeti, Kyela Mjini, Ikolosheni, Itungi na Ipyana: Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili mradi huo uanze kujengwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Suma Fyandomo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mradi wa Kiwira, tayari umeanza kushughulikiwa. Kuhusu mkandarasi kutoonekana site, lakini kuna kazi za awali tayari zimeshaanza na suala la kupeleka hela kwenye mradi wa Kyela Kasumulu, huu mradi tumeshaupelekea hela mara nyingi na tutaendelea kuupelekea kadiri tunavyopata fedha.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kukamilisha Ujenzi wa Mradi wa maji Tukuyu Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafsi ya kuuliza swali la nyongeza. Mradi wa Lunyinya – Chanya na Mradi wa Kilela – Rutungu – Lusungiro, miradi hii imesimama kwa muda mrefu kwa sababu mkandarasi hajalipwa. Ni lini mkandarasi atalipwa ili miradi hii iweze kukamilika? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji hivi vyote alivyovitaja vina miradi miwili, hii miradi ni kweli tayari imeanza kufanyiwa kazi na malipo yanaendelea kufanyiwa kazi. Tayari fedha zimepatikana wiki iliyopita, baadhi ya wakandarasi tunaanza kuwapunguza, kuwalipa. Hivyo, mkandarasi huyu pia tunatarajia aweze kulipwa fedha yake.