Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 51 2023-04-11

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kukamilisha Ujenzi wa Mradi wa maji Tukuyu Mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkataba wa ujenzi wa Mradi wa Maji Tukuyu Mjini ni wa miaka miwili na ulianza mwezi Agosti, 2021 na unatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2023. Hadi sasa utekelezaji unaendelea na umefikia asilimia 82. Kazi zilizokamilika ni pamoja na ujenzi wa banio katika chanzo, ulazaji wa bomba kuu lenye urefu Kilomita 9.5, ujenzi tanki moja lenye ujanzo wa lita milioni 1.5 na ulazaji wa mtandao wa bomba wa umbali kilomita 20.