Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kufunga mtandao wa Wi-Fi maeneo yote nchini kufuatia jamii kuhamasika na matumizi ya teknolojia?

Supplementary Question 1

MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia hamasa kubwa iliyofanywa na Serikali kuhusu matumizi ya teknolojia iliyosababisha wananchi wengi kutumia mtandao wa internet: Je, Serikali haioni haja sasa ya kuwa na bundle maalum kwa ajili ya wajasiriamali wadogo litakalowasaidia kutafuta masoko kwa njia ya mtandao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Ni lini sasa Serikali itahakikisha taasisi zote za elimu zinakuwa na huduma ya Wi- Fi itayaowasaidia walimu na wanafunzi kuongeza maarifa, na vilevile kutoa mchango wao katika ulimwengu wa elimu duniani? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Mheshimiwa Mbunge alishaleta maombi yake kuhusu vikundi na vikoba kwa ajili ya kupata bundle maalum. Ni kweli kabisa kwamba, huwa tuna utaratibu kama maeneo ya vyuoni, na maeneo mbalimbali ambayo huwa yanapata special offer. Hilo tumeshalipokea na Serikali bado inalifanyia kazi, na pale ambapo tutakuwa tumekamilisha, basi tutamjulisha Mheshimiwa Mbunge kwa ajili ya hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipengele cha pili; ni wazi kabisa kwamba huu ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Ibara ya 61 (h), inayotutaka kuanzisha huduma ya mawasiliano ya internet ya kasi katika maeneo yote ya umma (Public Place) ikiwemo maeneo ya hospitali, taasisi za elimu na vituo vya usafiri hadi kufikia asilimia 40 mwaka 2025.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari Serikali imeshaanza. Kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi, tumeshajenga vituo sita, na mwaka huu tayari kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa wote, tumejipanga kwa ajili ya kwenda kufikisha huduma ya internet ya Wi-Fi katika maeneo 20 na tutaendelea kufanya hivyo mpaka tutakapofikia katika lengo la Serikali ambalo ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi kufikia asilimia 40.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.