Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 50 2023-04-11

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kufunga mtandao wa Wi-Fi maeneo yote nchini kufuatia jamii kuhamasika na matumizi ya teknolojia?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kufunga mtandao wa Wi-Fi maeneo yote ya umma nchini kufuatia jamii kuhamasika na matumizi ya teknolojia katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa utekelezaji wa kufunga mtandao wa Wi-Fi umefanyika katika vituo sita ambavyo vinatoa huduma ya internet ya wazi (Internet hotspot) katika maeneo mbalimbali. Maeneo hayo ni Stendi ya Nanenane, Dodoma; Buhongwa, Mwanza; Kiembesamaki, Unguja; Chuo Kikuu cha Dodoma, Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu (CIVE) na Soko la Tabora, na Chuo cha Ustawi wa Jamii Lungemba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji huo utaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini kwa kutegemea upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.