Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN M. SALLU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, kwa hiyo wananchi wa Handeni tunategemea hivi karibuni michakato itaanza, nina swali moja la nyongeza.

Barabara itokayo Chalinze mpaka Segera, hasa kile kipande kinachoanzia Manga mpaka Segera zinatokea ajali nyingi sana na kupoteza nguvu kazi kubwa sana ya nchi hii, na sababu kubwa ni wembamba wa barabara na kona nyingi.

Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kufanya maboresho kwenye barabara hiyo ili tuweze kuondoa vifo hivi vya wananchi wa kitanzania na majeruhi? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa John Marko Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mhshimia Mwenyekiti, barabara ya Chalinze hadi Segera ni barabara ambazo ni barabara standard kwa maana ina upana wa mita 6.5 kwa maana kila upande mita 3.25 na hizo ndiyo barabara zilizo nyingi. Ninatambua kwamba ni kweli kuna ajali nyingi zinataokea lakini ambacho tumekifanya tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya economic study na usanifu wa barabara hiyo kwenye maeneo ya miinuko, kona na kuhakikisha kwamba barabara hii ipanuliwe hasa kwenye maeneo ambayo watu wameongezeka kwenye vijiji na kuongeza upana wa mabega.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafanya economic study na feasibility study ambayo tutaanza mara moja kwa ajili ya kupunguza ajali ili watu waweze kuonana kwa umbali, ni barabara ambayo imeinuka sana, ukilinganisha na yaani embankment yake ni ya juu. Kwa hiyo, hilo tumeshaliona na Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kufanya hiyo study na economic study. Ahsante.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Kibosho Shine, Kwa Raphael hadi International School kwa kiwango cha lami kwani ni kipande kidogo kimebakia?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema kipande kilichobaki kidogo nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua kazi kubwa imeshafanyika na tunatafuta fedha kuweza kukikamilisha hicho kipande kilichobaki cha barabara ili wananchi waweze kupata huduma ambayo imekusudiwa na Serikali. Ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga au kuboresha barabara inayotoka Chuo cha Diplomasia Kurasini kupitia Tom Estate kupitia Msikitini ka Mzuzuri mpaka kuunganisha na barabara ya Mandela? Kipande hicho ni korofi, makontena yanapita kwa shida sana ukiwa na gari ndogo unaweza ukafikiria sasa kontena linaniangukia, nashukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kisangi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri tu kwamba sijaielewa vizuri hiyo barabara aliyoitaja lakini nimuombe pia Mheshimiwa Mbunge, kama ataridhia basi niweze kukutana naye ili niweze kuielewa hiyo barabara ili niweze kumpa hasa majibu sahihi badala ya kujibu tu. Sijaielewa vizuri hiyo barabara, ahsante.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumWuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, hiyo barabara ya Iringa Bypass ni mwaka wa tatu sasa tangu imejengwa na imeanza kubomoka.

Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Iringa Bypass?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jesca Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii yenye urefu wa kilometa saba tumeshaanza kuijenga. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Iringa na watu wote wanaopita hiyo barabara, Serikali inatambua ni barabara muhimu sana kwani, pale kwenye barabara pakifunga, hatuna njia. Namwomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira, kwenye bajeti hii tuna hakika tutaendelea kuijenga kwa awamu ili tuweze kuikamilisha na tuwe na barabara ambayo ni bypass kwa Mji wa Iringa, ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 5

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sera ya Wizara hii inaelekeza kuunganisha barabara ya Mkoa mmoja na Mkoa mwingine kwa kiwango cha lami. Tuna barabara mbili kutoka Karatu kwenda Mbulu ambapo ni Mkoa wa Manyara na Mkoa wa Arusha; na kuna barabara inayotoka Karatu – Njiapanda – Mang’ola – Lalago ambayo inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu, zote hizi hazijajengwa kwa kiwango cha lami: Je, lini Serikali mtakamilisha barabara hizi au mtajenga barabara hizi kwa kiwango cha lami ikiwa sera yenu inaelekeza hivyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Paresso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli sera ni kuunganisha barabara kwa kiwango cha lami Mkoa na Mkoa, lakini kipaumbele pia ni kuhakikisha kwamba, kama barabara ambazo zinakwenda parallel tutaanza na moja halafu itafuata nyingine kulingana na upatikanaji wa fedha. Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba barabara ya Oldeani – Mang’ola kwenda Matala - Sibiti inakwenda kama parallel, yaani sambamba na barabara ya Karatu –
Mbulu – Hydom – Kidarafa hadi Sibiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo barabara ambayo tunaita Serengere Southern Bypass imeingizwa kwenye mpango wa kuijenga kwa EPC + F, lakini Serikali inafikiria kuijenga barabara kuanzia Oldeani hadi Mang’ola kwa kiwango cha lami kabla ya kupita Mang’ola kwenda Sibiti, ahsante.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 6

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Serikali iliahidi kuanza kujenga barabara ya Mafinga – Mgololo ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa letu. Tunashukuru kwa sababu, tayari wamesema itaanza kujengwa: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali ni: Je, ni lini mchakato wa EPC + F utakamilika ili barabara ya Mafinga – Mgololo ianze kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mafinga kwenda Mgololo imeingizwa kwenye Mpango wa EPC + F. Kama Wizara, upande wa ufundi kwa maana ya engineering, yaani Engingeering Procurement na Construction, tumeshakamilisha, na sasa ziko zinachakatwa na Wizara ya Fedha, na baada ya hapo basi taratibu zinazofuata za manunuzi zitaanza, ahsante.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 7

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia fursa hii. Swali langu kwa Wizara ni kwamba, Mkoa wa Mtwara na Barabara yake ya kiuchumi kilometa 210 kutoka Mtwara – Tandahimba – Newala – Masasi ambayo tayari imeshajengwa kilometa 50 na fedha zimeshapatikana kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika muda mrefu, lakini kila tukiuliza tunaambiwa Serikali ipo kwenye mchakato wa manunuzi. Sasa tunataka kujua, ni lini mchakato wa manunuzi utakamilika ili barabara hii ya kiuchumi ianze kujengwa? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Newala, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara ya Mnivata – Tandahimba – Newala hadi Masasi, kilometa 160 ipo kwenye taratibu za manunuzi. ADB wameshakubali, tumepata no objection; kwa hiyo, kinachoendelea sasa hivi ni taratibu za kawaida za manunuzi na hasa tunapokuwa tunashirikiana na wenzetu wahisani kwamba, tutakapokamilisha lot hizi mbili, zitaanza kujengwa. Tuna uhakika kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha huu, shughuli nyingi zitakuwa zimeanza katika hiyo barabara, ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Supplementary Question 8

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kuuliza: Je, ni lini sasa Serikali itamaliza ujenzi wa barabara ya Chang’ombe inayoanzia mataa ya Chang’ombe kuelekea barabara ya Kilwa; ukilinganisha kwamba, sasa hivi kuna foleni kubwa sana na ile barabara ni kubwa na hasa ukizingatia wananchi wengi wanapita; na hasa kipindi ambacho kuna michezo kwenye uwanja ule wa Taifa, hasa Simba na Yanga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilave, Mbunge wa Temeke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Chang’ombe kwenda Kilwa ni sehemu ya barabara za BRT Awamu ya Pili. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, naye atakuwa shahidi kwamba kasi imeongezeka sana. Tuna uhakika, kwa mujibu wa kazi anavyoendelea mkandarasi huyu, barabara hii itakamilishwa kama tulivyokubaliananaye kwenye mkataba, ahsante.