Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 48 2023-04-11

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi kwa kiwango cha lami kipande cha barabara ya Turiani hadi Handeni kilometa 104?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Marko Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii inayoanzia Magole, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya kuanzia Magole hadi Turiani yenye urefu wa kilometa 45.27, katika mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya shilingi bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi wa sehemu iliyobaki kati ya Turiani – Mziha hadi Handeni kilometa 104 kwa awamu, ahsante.