Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha elimu inayotolewa inaendana na mahitaji ya sasa?

Supplementary Question 1

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu suala la elimu ni suala nyeti katika Taifa letu, ni muda sasa Serikali imesema ipo kwenye mchakato wa mapitio na watoto wetu wanaendelea kutumia mtaala huu ambao hauna tija kwao. Ni lini hasa utekelezaji utaanza rasmi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, vijana wengi wameathiriwa na mfumo huu ambao hauna tija, wengi wapo mtaani na wanashindwa afanye nini kwa elimu walioipata. Je, ni upi mkakati wa Serikali wa kuwasaidia vijana hawa ambao tayari ni wahanga wa mfumo wetu huu wa elimu pale tutakapobadilisha mfumo rasmi. Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sylvia, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwishaeleza kwenye majibu ya swali la msingi kwamba kwa upande wa upitiaji wa mitaala Serikali tayari tumekamilisha rasimu ya mitaala pamoja na sera yetu, hivi sasa tupo katika hatua za kurudisha tena kwa wadau lakini vilevile katika mamlaka mbalimbali ambazo zitathibitisha au zita- approve mitaala hiyo. Mara tu mchakato huo utakapokuwa umekamilika tunataraji mitaala hii itaanza kutumika rasmi kwenye ngazi zote za elimu hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali lake la pili, anazungumzia kwamba tayari kuna wananfunzi ambao walitumia mitaala ile ya zamani. Naomba nimuhakiishie tu Mheshimiwa Mbunge, utaratibu wa upitiaji wa mitaala pamoja na sera ni suala endelevu ni suala ambalo linatokea mara kwa mara pale tunapoona tu kuna mahitajji ya mabadiliko ya mitaala pamoja na sera, Serikali imekua ikifanya hivyo ili elimu inayotolewa ilingane au iendane na mazingira halisi ya kazi au mazingira halisi ya dunia inavyokwenda. Vilevile utaratibu wetu au sera yetu ya elimu inampa wasaha yule mhitimu kuweza kujiendeleza au kwenda maeneo mengine na kupata elimu zaidi ambayo itaendana na mazingira yale ambayo anafanyia kazi. Ninakushukuru sana.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: - Je, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha elimu inayotolewa inaendana na mahitaji ya sasa?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, kwa kuwa kumekuwepo na changamoto katika Shule za Msingi na Sekondari kwa ajili ya watoto kupata chakula shuleni. Nini kauli ya Serikali kuhusu watoto kupata chakula shuleni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba watoto wanakuwa kwenye ufanisi mzuri kiakili na kimwili?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli suala la chakula shuleni kwa watoto ni jambo ambalo ni muhimu, bado kuna changamoto kubwa sana ya upatikanaji chakula mashuleni kwa ajili ya watoto wetu. Serikali tulishatoa mwongozo wa namna gani wazazi au walezi wanaweza kushirikiana na Serikali kuhakikisha kwamba watoto wetu wanapata chakula shuleni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia mwongozo ule unadadavua na unatoa maelekezo mazuri kabisa kwamba kila upande ni namna gani unaweza kushiriki ili wanafunzi wetu waweze kupata chakula wanapokuwa shuleni. Nakushukuru sana.