Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 47 2023-04-11

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: -

Je, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha elimu inayotolewa inaendana na mahitaji ya sasa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sylvia Francis Sigula, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali inaendelea na mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, sambamba na mapitio ya Mitaala ya Elimu katika ngazi zote.

Mabadiliko haya ya Sera na Mitaala yamelenga kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa stadi za kazi, stadi za maisha za karne ya 21 ambazo ni fikra tunduizi, ubunifu, ushirikiano, uongozi pamoja na stadi za mawasiliano na teknolojia ya habari kwa lengo la kuwajengea uwezo wahitimu kukabiliana na mabadiliko mbalimbali yanayotokea katika jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali upande wa Vyuo vya Kati na Vyuo vya Ufundi Stadi, Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTVET) linaendelea na maandalizi ya Occupational/Professional Standards ambazo zitatoa mwogozo katika mabadiliko na maandalizi ya mitaala inayokidhi mahitaji ya sasa na baadae. Vilevile, kwa upande wa Elimu ya Juu tayari Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) inaendelea kukusanya maoni ya wadau kuhusu ubora wa elimu inayotolewa na Vyuo Vikuu pamoja na kutoa mafunzo kwa Wahadhiri katika maandalizi ya mitaala inayozingatia mahitaji ya ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.