Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Mji Bunda?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakshukuru. Je, udahili wa wanafunzi kuingia VETA mpya iliyojengwa Wilayani Longido Mkoa wa Arusha unaanza lini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vyuo 25 vya Wilaya, vile ambavyo tulijenga katika mwaka uliopita wa fedha, ambapo ukamilishaji wake hivi sasa ndio tunakwenda kukamilisha, tunatarajia udahili ule wa kozi zile za muda mrefu kuanza mwezi wa Kumi mwaka huu, ila zile kozi za muda mfupi muda wowote kuanzia mwezi wa Sita zinaweza zikaanza rasmi.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Mji Bunda?

Supplementary Question 2

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa kila Wilaya imeandikiwa kupata chuo cha VETA. Je, ni lini Serikali itaboresha chuo cha VETA Buhongwa ili kiwe na hadhi ya chuo cha VETA katika Wilaya ya Nyamagana?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Matondo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwanza tunakwenda kujenga kwenye maeneo ambayo hayana huduma au hayana vyuo hivyo, lakini kwenye maeneo ambayo vyuo tayari vipo ni azma vilevile ya Serikali kuhakikisha kwamba, vyuo vile tunakwenda kuviboresha kwa maana ya kufanya ukarabati lakini vilevile kuongeza miundombinu. Nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu, kwamba Serikali inaandaa bajeti kila mwaka ile ya kufanya maendelezo kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo na chuo hiki ambacho amekitaja Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Mji Bunda?

Supplementary Question 3

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa, Serikali yetu na nchi yetu inajikita zaidi katika matumizi ya teknolojia na TEHAMA. Je, Serikali ni lini itaona ni wakati muafaka wa kuongeza masomo haya ya sayansi ikiwemo hisabati kwa wanafunzi wanaofanya masomo ya HGKL. Ni ni lini ili kuwafanya watu hawa wawe tayari katika soko la ulimwengu na Tanzania?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Asha Mshua kama ifuatavyo: -

Mhehsimiwa Mwenyekiti, masomo ya hisabati pamoja na teknolojia tayari yapo kwenye mitaala yetu lakini naomba tu nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, hivi sasa tunafanya mapitio ya mitaala katika ngazi zote za elimu ambapo tutazingatia hasahasa kwenye maeneo haya ya sayansi pamoja na teknolojia na tunaamini kabisa kwa mwendo huo tunaokwenda nao swali lake litakuwa limepata majibu ya jumla na ya moja kwa moja.