Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 46 2023-04-11

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. ROBERT C. MABOTO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Halmashauri ya Mji Bunda?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Robert Chacha Maboto, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kujenga Chuo cha Ufundi Stadi katika kila Mkoa na Wilaya nchini. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga kiasi cha Shilingi za Kitanzania Bilioni 100 kwa ajili ya kujenga Vyuo vya Ufundi Stadi katika Wilaya 64 ambazo zilikuwa hazijajengewa vyuo hivyo. Tayari Serikali imeshakamilisha kuandaa michoro na upatikanaji wa maeneo kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Bunda ni miongoni mwa Wilaya 64 ambazo zipo katika mpango wa kuanza kujengewa Vyuo vya Ufundi Stadi katika mwaka huu wa fedha ambapo tayari kiasi cha Shilingi Milioni 45 kimetolewa mwezi Machi, 2023 kwa ajili ya shughuli za awali ikiwemo upimaji wa udongo kwa ajili ya uhimilivu pamoja na tathmini ya athari za mazingira na jamii wakati wa ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.