Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Umeme wa Nguvu ya Jua utaanza kutekelezwa katika Kata ya Talaga Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napongeza Serikali kwa majibu mazuri juu ya hatua ya mwendelezo wa Mradi huu muhimu wa uzalishaji wa umeme wa jua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni moja tu la nyongeza, kwamba ni kwa namna gani zana ya ushirikishwaji wa jamii inayohusika na hasa juu ya masuala ya fidia, imekuwa ikizingatiwa lakini pia suala zima la uongozi hasa wa ngazi za chini Serikali za Mitaa umekuwa ukihusishwa hili kuona kwamba michakato ya haki na tathmini iliyo halali kwa ajili ya malipo kwa wananchi inazingatiwa? Naomba kujibiwa.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Butondo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Butondo kwa kulifuatilia jambo hili mara kwa mara, lakini namhakikishia kwamba kama anavyofahamu na anavyoona limefikia mwisho na mambo yanakwenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jibu la msingi nimesema malipo ya fidia yataanza kufanyika mwishoni mwa mwezi huu, lakini taratibu zote zote za fidia zimepitiwa kama ambavyo zinaelekezwa na sheria. Kwa hiyo wale wataoathirika wote tayari wamebainishwa na wameshirikishwa katika mchakato huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo jambo zuri sana ambalo naomba kulisema kwa sababu ya uhitaji mkubwa wa umeme tuliokuwanao tumekubaliana na wenzetu wa TANESCO na Serikali imewaagiza watoe pesa zao kwanza kuanza kulipa fidia haraka kama mkopo, halafu badae Wizara ya Fedha itakapokuwa imelipwa watarudishiwa kwenye eneo lao. Kwa hiyo wiki hii ambayo tumeianza jana wananchi kule wataanza kulipwa fidia katika mazingira yao ili kuhakikisha kwamba mradi hii unakimbizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaelekeza wenzetu wa TANESCO watakapoenda kulipa fidia kupitia halmashauri, kupitia Serikali za Vijiji na Viongozi wetu wa Serikali waliokuwa nao washirikiane hili kuwabaini wale ambao ni waathirika halisi na waweze kupewa haki yao stahiki kwa mujibu wa sheria hili mradi uweze kutekelezwa bila tatizo lolote.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Mradi wa Umeme wa Nguvu ya Jua utaanza kutekelezwa katika Kata ya Talaga Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa kunipa nafasi. Mradi wa REA wa vijiji 26 Wilaya ya Tanganyika ambao Mheshimiwa Naibu Waziri, alikuja akauzindia mpaka sasa haujakamilika. Je, ni lini Serikali itakamilisha ule mradi ili uweze kuleta tija kwa wananchi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Selemani Kakoso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilienda kuzindua Mradi huo mimi mwenyewe na Mkandarasi anayetekeleza Mradi huo Mkandarasi wa ITIBIKO bado anaendelea na kazi site na makubaliano tuliyokuwanayo ni kufikia Desemba mwaka huu mradi huu pamoja na miradi mingine yote ya kupeleka umeme vijijini iwe imekamilika. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Kakoso kwamba jambo hili tunalifuatilia na kabla ya mwaka huu kwisha tutahakikisha ya kwamba kazi hiyo inakamilika katika eneo lake la Wilaya ya Tanganyika lakini na maeneo mengine.