Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 43 2023-04-11

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, ni lini Mradi wa Umeme wa Nguvu ya Jua utaanza kutekelezwa katika Kata ya Talaga Wilayani Kishapu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ujenzi wa Mradi wa Umeme wa Jua katika Kijiji cha Ngunga, Kata ya Talaga, Wilayani Kishapu unalenga kuzalisha umeme kwa kutumia jua kiasi cha megawati 150 kwa gharama za Euro milioni 115.30 ambayo itakuwa ni megawatIi 50 na Euro milioni 42 kwa awamu ya kwanza na megawati 100 kwa Euro milioni 62 kwa awamu ya pili. Fedha za awamu ya kwanza tayari zimepatikana, taratibu za kumpata Mkandarasi Mshauri na Mjenzi zipo katika hatua za mwisho. Fedha ya awamu ya pili inaendelea kutafutwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malipo kwa ajili ya fidia kwa wananchi wa Kijiji cha Ngunga watakaoathirika na mradi, kiasi cha shilingi bilioni 1,825 kitaanza kulipwa mwishoni mwa mwezi Aprili, 2023 na Ujenzi wa Mradi huu (awamu ya kwanza) utatekelezwa kwa kipindi cha miezi kumi na nne (14) kuanzia mwezi Juni, 2023, baada ya kukamilisha taratibu za manunuzi ya wakandarasi na malipo ya fidia.