Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini jengo la Manispaa ya Mtwara Mikindani litajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina swali moja la nyongeza. Iliundwa tume ya kuja kuangalia jengo lile la Mtwara tangu mwaka 2020 na tume ile ikapendekeza kwamba jengo lile lisitumike;

Je, ni lini sasa Seriali itaamua kutuletea fedha ili tuweze kupanga sehemu nyingine kwa sababu jengo lile haliko salama sasa kwa wafanyakazi waliopo mule ndani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua kwamba jengo lile ni la siku nyingi na ni chakavu na kwa kweli halina sifa ya kuendelea kutumika kama jengo la halmashauri. Hivyo, Serikali imeweka kipaumbele baada ya kukamilisha majengo haya ambayo mengi yako katika hatua za ukamilishaji katika halmashauri zile mpya, tutakwenda kwenye halmashauri kongwe ikiwepo Halmashauri ya Mtwara Mikindani na nimwakikishie kwamba tutahakikisha kwamba Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo hilo, ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini jengo la Manispaa ya Mtwara Mikindani litajengwa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ni halmashauri kongwe na jengo la utawala halijakamilika. Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa jengo la utawala Halmashauri ya Shinyanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali ilipeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga. Tunafahamu jengo lile halijakamilika, lakini ujenzi huu unakwenda kwa awamu. Awamu ya kwanza fedha zimepelekwa na kazi ya ujenzi imeanza. Nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatafuta fedha ili ipeleke awamu ya pili kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo hilo, ahsante.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini jengo la Manispaa ya Mtwara Mikindani litajengwa?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jengo la Halmashauri ya Rungwe ni jengo la muda mrefu sana.

Ni lini Serikali itatupatia fedha angalau kufanya ukarabati na kuongezea baadhi ya vyumba ili kuwawezesha wafanyakazi wafanye kazi vizuri?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilitoa maelekezo kwa wakurugenzi wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa kwamba pamoja na kutegemea fedha kutoka Serikali kuu lakini wanao wajibu wa kutenga fedha kupitia mapato ya ndani kwa ajili ya ukarabati mdogo mdogo pia kuongeza vyumba viwili, vitatu katika majengo ya utawala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa nina uhakika kwamba Halmashauri ya Rungwe wana uwezo wa kufanya ukarabati wa majengo yale nitumie fursa hii kumwelekeza Mkurugenzi kuanza kuweka kipaumbele kwa awamu kwa ajili ya ukarabati wa majengo ya halmashauri na pia kuongeza vyumba vichache ambavyo vinahitajika, ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini jengo la Manispaa ya Mtwara Mikindani litajengwa?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Natambua Serikali imekuwa ikitenga fedha katika ujenzi wa hospitali wa halmashauri ya Mji wa Bunda. Sasa ningependa kusikia kwa mwaka huu wa fedha nini tamko la Serikali ili hospitali ile iweze kumalizika haraka?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa hospitali za halmashauri ikiwemo hospitali ya Halmashauri ya Bunda unakwenda kwa awamu. Kuna awamu ya kwanza ambapo fedha zilipelekwa, awamu ya pili majengo yapo yaliyokamilika na yako ambayo hayajakamilika. Nimhakikishie kwamba Serikali imeweka mpango mkakati wa kuhakikisha inatafuta fedha kwa awamu zinazofuata ili hospitali hizi zote zikamilike na kuwa na miundombinu inayotakiwa kutoa huduma kwa wananchi na hospitali hii ya Bunda pia itapewa kipaumbele.