Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 40 2023-04-11

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: -

Je, ni lini jengo la Manispaa ya Mtwara Mikindani litajengwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jengo la Utawala la Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara – Mikindani lilijengwa mwaka 1948. Hivyo, jengo hilo limechakaa na halitoshelezi mahitaji ya Ofisi. Serikali inatambua umuhimu wa Halmashauri hiyo kujengewa jengo jipya kwa matumizi ya Ofisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Novemba, 2022 Halmashauri iliwasilisha maombi ya kutengewa bajeti katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala na nyumba ya Mkurugenzi. Serikali itatenga bajeti ya shilingi milioni 180 katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya ujenzi wa Nyumba ya Mkurugenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele cha kukamilisha majengo ya utawala yaliyoanza kujengwa kisha itaendelea na ujenzi wa majengo mapya ya utawala likiwemo jengo la Halmashauri ya Mtwara Mikindani. Ahsante.