Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Manoleo hadi Kituo cha Afya Upuge itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali; nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, Serikali iko tayari kukipa kipaumbele kipande kile cha kilomita nne kutoka barabara kuu ya Nzega kwenda kituoni ili kiweze kufikika wakati wa dharura?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Je, Serikali sasa iko tayari kumalizia kipande cha barabara kinachotokea pale kituo cha afya kwenda Kijiji cha Kasenga, Majengo, Ikongolo, Ipuge; vilevile vijiji vya Izugawima, na Nzuguka ili wananchi wa vijiji vile waweze kupata huduma haraka kwenye Kituo cha Afya cha Upuge?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iko tayari kuipa kipaumbele barabara hiyo ya kilomita nne ili kuweza kusogeza huduma za jamii kwa wananchi. Nimwelekeze Meneja wa TARURA wa Halmashauri ya Uyuwi kuhakikisha kwamba wanatenga fedha kwenye eneo hilo, kwa maana ya kuipa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kwa kuwa barabara hii ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja, ambayo inaunganisha kituo cha afya na vijiji kadhaa alivyovitaja ni muhimu kuwawezesha wananchi kupata huduma za afya Serikali iko tayari kuipa kipaumbele barabara hii ili iweze kujengwa na kupitika vizuri. Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Manoleo hadi Kituo cha Afya Upuge itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, je, ni lini barabara ya Ihanda-Ipunga hadi Chinji itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilishawaelekeza mameneja wa TARURA katika wilaya zetu kuhakikisha wanatenga vipaumbele vya barabara ambazo zinahitaji kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo naomba nimwelekeze Meneja wa TARURA wa Wilaya hii ya Mbozi kuhakikisha kwamba wanaleta maombi hayo kama ni kipaumbele ili Serikali iweze kufanya tathmini na kuona uwezekano wa kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi huo, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Manoleo hadi Kituo cha Afya Upuge itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Lini Serikali itatenga fedha za kutosha ili barabara inayotoka Mtandika kwenda Ikula iweze kujengwa kwa sababu barabara ile ni hatarishi sana na wakati wa mvua haipitiki wanawake wajawazito wanapandishwa mshikaki kwenda katika kituo cha afya kujifungua?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii barabara ya kutoka Mtandika kwenda Igula na vijiji ambavyo amevitaja Mheshimiwa Mbunge ni kweli ni barabara muhimu na inapelekea wananchi kufika kwenye kituo cha afya kwa ajili ya huduma za afya. Kwa hivyo Serikali itaendelea kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika ili fedha iweze kutafutwa na kuiboresha barabara hiyo ili kipindi cha masika iweze kupitika vizuri na wananchi waweze kupata huduma nzuri za usafiri, ahsante.