Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 39 2023-04-11

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: -

Je, ni lini Barabara ya Manoleo hadi Kituo cha Afya Upuge itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Manoleo - Kituo cha Afya Upuge yenye urefu wa kilometa 22.10 imesajiliwa kwa jina la Nyambele – Upuge – Muhogwe - Magiri ambapo kutokana na umuhimu wake imeendelea kutunzwa kwa kuwekewa kipaumbele kwenye bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na umuhimu wa barabara hii, Serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe kilometa 13 na kujenga makalavati saba, ambapo ipo hatua ya uandaaji wa nyaraka za zabuni kwa ajili ya kumpata Mkandarasi. Ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi Mei, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili Barabara ya Nyambele – Upuge – Muhogwe – Magiri yenye urefu wa kilometa 22.10 iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Aidha, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itatenga shilingi milioni 91.8 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida kilometa 15, ujenzi kwa kiwango cha changarawe kilomita mbili na kunyanyua tuta na kujenga makalvati mawili, ahsante.