Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza msongamano wa watu wanaofuatilia hati za kusafiria?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI MAKAME MLENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mbali na majibu mazuri ya Serikali naomba niulize masuala mawili ya nyongeza. Kwa kuwa watoa hati ni wanadamu na wanadamu wana kawaida ya wakati mwingine kukosea. Inapotokea kukosea wakati wa kutoa hati (printing error) na wakati huo wale wapewa hati wanakuwa wameshalipa. Kwa nini idara inawalipisha tena watu wale wakati wao Uhamiaji ndiyo wamekosea?

Mheshimiwa Spika, swali la pili Je, Serikali ipo tayari kutoa tamko kupitia Waziri la kwamba suala hili wapewa hati hawatalazimika kulipishwa mara ya pili badala yake gharama hizi wachukue Idara? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Haji Makame Mlenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna wakati makosa hufanyika lakini makosa yakichunguzwa yakionekana aliyechangia kufanya makosa haya ni yule mwombaji kwa sababu ya taarifa alizojaza basi mwombaji huyo lazima atalipa. Lakini ikiwa itathibitika kwamba makosa hayo yanatokana na waandaaji ambao ni watumishi wa Idara ya Uhamiaji basi tutaangalia uzito wake ili waweze kufidia wenyewe utoaji wa hati hizo mpya. Nashukuru.