Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 24 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 215 2022-05-17

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza msongamano wa watu wanaofuatilia hati za kusafiria?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Haji Makame Mlenge, Mbunge wa Chwaka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Idara ya Uhamiaji katika kupunguza msongamano wa waombaji wa Hati za kusafiria, imefunga mifumo ya kielektroniki ya utoaji wa hati za kusafiria katika Mikoa yote ya Zanzibar. Ufungwaji wa mifumo hiyo kumeondosha msongamano kwa wananchi katika Ofisi Kuu kwani kwa sasa wananchi wanaweza kuomba na kufuatilia maombi ya Hati za kusafiria katika Mkoa wowote anaoishi. Nashukuru.