Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: - Je, ni lini mradi wa visima vitatu katika Kijiji cha Turuki utakamilika kwa ajili ya kupeleka maji Liwale Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza napenda kutoa shukrani za dhati kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia matumaini, lakini hata hivyo namshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanznaia, Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan, tumepata fedha zile za UVIKO, tumejenga chujio na sasa hivi tunapata maji safi ka Mji wetu wa Liwale. Nina swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, vipo Vijiji vya Ngongowele, Makata, Mtatawa, Kihangala, Kipelele, Nguta, Mpengele, Ndapaka, Mlembwe na Nangano. Vijiji hivi bado havijapata maji safi na salama. Naomba kupata comfort kutoka Serikalini, ni lini wananchi wa vijiji hivi wataweza kufikiwa na mradi wa maji ili kutimiza ile azma ya kumtua Mama ndoo kichwani iweze kukamilika? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Kuchauka Zuberi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, napenda kupokea shukrani zake na vile vile tumuombee Mheshimiwa Rais, kwa ababu adhma ya kumtua Mama ndoo kichwani hakika inatekelezwa maeneo yote.
Mheshimiwa Spika, vijiji alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge tayari RUWASA Mkoa inafanyiakazi na mwaka ujao wa fedha tutavifikia kwa kila kijiji, kila tunapopata fedha kuhakikisha maeneo yote ya Liwale yanakwenda kupata maji safi na salama.