Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 29 2023-04-05

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -

Je, ni lini mradi wa visima vitatu katika Kijiji cha Turuki utakamilika kwa ajili ya kupeleka maji Liwale Mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Liwale katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 Serikali imechimba visima vitatu katika Kijiji cha Turuki. Visima hivyo kwa pamoja vina uwezo wa kuzalisha lita 1,008,000 kwa siku na vitaongeza uzalishaji wa maji kutoka lita 1,200,000 kwa siku hadi kufikia lita 2,208,000 kwa siku.

Mheshimiwa Spika, usanifu kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji hayo ulikamilika mwezi Machi, 2023 na ujenzi umepangwa kutekelezwa na kukamilika katika mwaka wa fedha 2023/2024. Kazi zitakazofanyika ni pamoja na ulazaji wa mtandao wa bomba umbali wa kilomita 78 na ujenzi wa matanki mawili (2) yenye ujanzo wa lita 1,300,000.