Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuongeza viwanda vya kusindika ngozi za mbuzi na ng’ombe?

Supplementary Question 1

MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza ninaishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa bado mahitaji ni makubwa ya wananchi hao wajasiriamali ambao wanajishughulisha na biashara ya ngozi ya mbuzi na ng’ombe, hasa tukizingatia kwamba wananchi wengi wana mahitaji makubwa lakini tunanunua nje. Kwa mfano, mikoba ya kike ambayo ni hand bag, viatu pia mikanda ya akina Baba.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza nguvu ya viwanda ili vifaa hivi sasa viwe vina ubora katika nchi yetu?

Swali la pili, pamoja na kuwa umesema mnatafuta uwekezaji labda mtuambie Serikali viwanda vingapi ambavyo kwa sasa vipo, katika nchi yetu vinavyojishughulisha na usindikaji wa ngozi ya mbuzi na ng’ombe?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asya Sharif, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mahitaji ya ngozi ambazo zipo katika hatua ya mwisho kwa maana finished leather kwa ajili ya bidhaa za ngozi ikiwemo mikoba na viatu bado ni changamoto katika viwanda vyetu vya ndani. Moja ya mikakati tuliyonayo ni kuhakikisha tunawahamasisha kwanza wafugaji kuzalisha ngozi zinazokidhi mahitahji, ikiwa ni pamoja na kuchunga mifugo yetu katika hali nzuri, ikiwa ni pamoja na kutokupiga chapa kuharibu ngozi, pia kupiga fimbo au viboko, mbuzi na kondoo.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili tunahamasisha uwekezaji katika viwanda hivi ambavyo vitatumia malighafi yetu kuzalisha bidhaa za ngozi kwa maana ya ngozi hadi mwisho (finished leather) kwa hiyo ni moja ya mikakati ambayo Seriakli inaendelea kufanya, katika kuhakikisha tunakuwa na ngozi nzuri.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na takwimu, tutamletea takwimu sahihi ya viwanda kwa sababu bado tunaendelea kuhamasisha na kuna viwanda vingi vidogo ambavyo vinaendelea kuzalisha bidhaa za ngozi katika nchi yetu, vikitumia ngozi kutoka ndani ya nchi lakini nyingine kutoka nje ya nchi. Ninakushukuru.