Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 28 2023-04-05

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kuongeza viwanda vya kusindika ngozi za mbuzi na ng’ombe?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asya Sharif Omar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa uwekezaji katika sekta ya ngozi unaongezeka. Mikakati hiyo ni pamoja na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi lakini Vilevile, Serikali katika kuhakikisha inavutia na kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya ngozi, imehakikisha viwanda vya ngozi vya ndani vinapata malighafi za kutosha hapa nchini kwa kuongeza ushuru kwa ngozi zinazouzwa nje ya nchi. Mfano, asilimia 80 kwa ngozi ghafi na asilimia 10 kwa ngozi iliyoongezwa thamani hadi kufikia kuwa ya “wet blue”. Aidha, Serikali imekuwa ikitoa vivutio mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kuvutia uwekezaji kama vile kusamehe kodi kwa mitambo inayoingizwa kutoka nje ya nchi kwa lengo la kusindika na kuzalisha ngozi na bidhaa za ngozi hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mikakati hiyo, Serikali inaendelea kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya ngozi kwa kuweka mazingira bora ya ufanyaji biashara nchini kupitia MKUMBI. Ninakushukuru.