Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha barabara zinazowapeleka Watalii Mlima Kilimanjaro?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa. Swali la kwanza; je, Serikali ina mpango gani wa kufungua VIP route ya Kibia ambayo hupeleka watu maalum kupanga Mlima Kilimanjaro ili tuweze kupata fedha za kigeni kama ambavyo tume-plan.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili mti mrefu kuliko yote Barani Afrika wenye mita 81.5 upo katika msitu wa Mlima Kilimanjaro katika Kijiji cha Pema, miundombinu ya kufika katika eneo hili na mazingira ya eneo hili ni mabaya. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha eneo hili ili tuweze kupata fedha za kigeni? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Profesa Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba tu nimtaarifu Mheshimiwa Profesa Patrick pamoja na wananchi wa Moshi kwamba kwa sasa hivi tayari Wizara imeshaanza ukarabati wa lango hili la VIP route ambapo lipo takribani asilimia sabini na kwa sasa tunatafuta Wawekezaji kwa ajili ya kujenga huduma za malazi na chakula. Pia kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024, tutajenga lango kuu linalopitia katika hiyo VIP route ambayo itawasaidia wageni kuingia katika Hifadhi ya KINAPA.

Mheshimiwa Spika, kwenye suala hili lingine mti mrefu zaidi hapa Afrika tumeshaanza kutenga kutenga fedha kwa ajili ya kuweka miundombinu sahihi katika eneo hilo ili Wataliii waweze kufika kwa urahisi. Kwa hiyo, kwa bajeti hii ambayo itapitishwa na Bunge lako hili tunatarajia kwamba zoezi hili litaanza kwa mwaka wa fedha unaokuja, ahsante. (Makofi)