Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 26 2023-04-05

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha barabara zinazowapeleka Watalii Mlima Kilimanjaro?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuweka kipaumbele na jitihada katika ukarabati wa barabara zinazotumika kupeleka watalii katika Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro kwa kushirikiana na wadau na mamlaka zinazohusika na utengenezaji na ukarabati wa barabara hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, miongoni mwa jitihada hizo zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa barabara za Machame, Mweka na Marangu kwa kiwango cha lami na ukarabati wa mara kwa mara wa barabara za changarawe zinazoelekea lango la Rongai, Lemosho, Kilema, Londorosi na Umbwe. Aidha, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 Serikali itafanya
ukarabati kwa kiwango cha changarawe kwa barabara inayoelekea kwenye lango la Umbwe.