Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE K.n.y. MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, ujenzi wa barabara ya njia nane kutoka Kibaha – Chalinze hadi Morogoro umefikia hatua gani?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya muuliza swali.

Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itakamilisha Barabara ya zamani kutoka Picha ya Ndege mpaka Mlandizi ili kupunguza foleni katika Barabara ya Morogoro?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Barabara ya Makofia - Mlandizi ni barabara ambayo ipo katika Ilani ya Chama kwa miaka mingi Je, ni lini Serikali itaanza kulipa fidia kwa wananchi wanaoishi katika maeneo haya kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi wa hiyo barabara? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mpango ni kuiboresha na kuipanua barabara mpya ambayo tunayo, kwa sasa tutaanza kufanya hiyo kazi ya kujenga barabara hizo nne badala ya kuanza na ile barabara ya zamani aliyotaja Mheshimiwa Mbunge. Nadhani kwa kufanya hivyo tutakuwa tumepunguza msongamano ambao upo na ndiyo lengo kubwa kuijenga ile barabara kwa njia nne zinazokwenda, zinazorudi lakini pia na zile zilizopo zitaendelea kuwepo.

Mheshimiwa Spika, suala la pili la Barabara ya Makofia – Mlandizi, Serikali sasa hivi inatafuta fidia ili kuwafidia wale wananchi ambao walishatathminiwa ambapo tuta-review tathmini na kuanza kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE K.n.y. MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza: - Je, ujenzi wa barabara ya njia nane kutoka Kibaha – Chalinze hadi Morogoro umefikia hatua gani?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Barabara ya Makambo – Songea barabara kubwa ya kiuchumi ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza na Mheshimiwa Deo Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii tayari imeshapata fedha kutoka World Bank ambapo tutaanzia mbele ya Njombe kuelekea Songea na kipande cha Njombe kuja Makambako Serikali inaendelea kutafuta fedha. Kwa hiyo sasa hivi tuko kwenye maandalizi ya kuanza kuitangaza ili ianze kujengwa kwa maana ya kukarabatiwa upya total rehabilitations, ahsante. (Makofi)