Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 24 2023-04-05

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE K.n.y. MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza: -

Je, ujenzi wa barabara ya njia nane kutoka Kibaha – Chalinze hadi Morogoro umefikia hatua gani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), imekamilisha upembuzi yakinifu wa awali kutathimini uwezekano wa kujenga barabara ya Kibaha – Chalinze – Morogoro yenye urefu wa kilomita 205 kwa utaratibu wa ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi. Matokeo ya utafiti huo yalionesha mradi kuwa na manufaa makubwa ya kiuchumi na kifedha iwapo itajengwa barabara ya njia nne ya kulipia katika ushoroba mwingine (new corridor). Barabara ya sasa inayotumika itaendelea kutumika na watumiaji ambao hawatakuwa tayari kupita katika barabara ya kulipia.

Mheshimiwa Spika, Mtaalam Elekezi ameanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali ili kumpata mwekezaji wa kufanya ujenzi wa barabara ya kiwango cha expressway yenye njia nne ambapo sehemu ya Kibaha – Mlandizi – Chalinze kilometa 78.9 imekamilika na kuidhinishwa na Wizara ya Fedha na Mipango tarehe 7/3/2023. Tangazo la kuwataka wazabuni kuonesha nia ya kuwekeza katika mradi huu limetolewa tarehe 14/3/2023 na mwisho ni tarehe 18/4/2023.

Mheshimiwa Spika, sehemu ya Chalinze hadi Morogoro kilomita126.1, upembuzi na usanifu wa awali unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2024, ahsante.