Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Lumpungu katika Jimbo la Muhambwe?

Supplementary Question 1

MHE: DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza maswali la nyongeza. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itaanzisha mchakato huo ili kuwasaidia kuchochea biashara ya ujirani mwema inayofanyika katika Kijiji hiki cha Kibuye katika Kata ya Kumsenga? (Makofi)

Mheshimiswa Spika, swali la pili; kwa kuwa Mto huo unatenganisha takribani vijiji sita vya Jimbo hili la Muhambwe na wananchi wanapita mipaka holela, je, Serikali haioni iko sababu ya kuharakisha mchakato huu wa daraja ili kuwe na mahali maalum pa kupita hili kudhibiti vitendo vya uhalifu katika Jimbo hili? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Florence George Samizi, Mbunge wa Muhambwe, kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, daraja hili halipo na linaunganisha nchi mbili, kwa hiyo ni daraja ambalo litahusisha wadau wengine si tu Burundi na Wizara ya Ujenzi, pia itahusisha Taasisi nyingine kama Ulinzi na Usalama, TAMISEMI, Ardhi, Wizara ya Fedha na Mambo ya Nje. Kwa hiyo, wadau wote hawa watakapokuwa wameona kuna haja thabiti ya kujenga na kuona inakidhi vigezo na sisi tukajiridhisha kama nchi, ndiyo tutaanza sasa kuwasiliana na wenzetu wa Burundi. Kwa hiyo sisi tumeshaanzisha huo mchakato kwa upande wetu kuona vigezo vyote vinakidhi, halafu tuweze kuwahusisha wenzetu wa Burundi, ahsante.