Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika kata ya Kala Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa sababu niliomba fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi Kala Kijiji cha Mpasa ambapo kuna biashara kubwa sana ya Samaki inafanyika. Ukanda wa Ziwa Tanganyika kuna uhalifu wa mara kwa mara hasa Kata ya Kizumbi;

Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha polisi Kata ya Kizumbi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo Mbunge wa Nkasi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunashukuru kwamba Mheshimiwa Mbogo amekuwa akitoa ushirikiano kwa Wizara yetu na wakati mwingine kupitia halmashauri yake amekuwa akitenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo hiki. Nimuahidi tu, baada ya kumaliza kituo hiki kadri hali ya fedha itakavyoruhusu maeneo tete kama ya Kizumbi tutaweza pia kuyajengea kituo cha polisi ngazi ya kata. Nashukuru.