Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 21 2023-04-05

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika kata ya Kala Wilayani Nkasi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Nkasi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetoa kiasi cha shilingi 115,809,000 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi Daraja C katika Kata ya Kala Tarafa ya Wampembe Wilaya ya Nkasi. Taratibu za ujenzi wa kituo tayari umeanza mwezi Machi, 2023. Kituo hiki kinajengwa eneo la Mpasa na kitahudumia vijiji vya Mpasa, Kala, Mlambo, Tundu, King’ombe na kilambo cha Mkolechi.